WAFUASI WA CHAMA CHA WANANCHI CUF WATINGA MAHAKAMANI.

 Ulinzi mkali wa polisi kwa watuhumiwa hao ambao walipelekwa rumande wakati mchakato wa dhamano yao ukifanyika ambao kila mmoja anatakiwa kusaini dhamana ya shilingi 100,000/= pamoja na mdhamini mmoja.
Ndugu na jamaa wakipata maelekezo kutoka kwa watuhumiwa hao.
Wanachama 30 wa Chama cha Wananchi CUF, leo wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam na kusomewa mashitaka matatu yanayo wakibili.

Washitakiwa hao waliofikishwa mbele ya Hakimu Mkazi, Emmilius Mchauru wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu walisomewa mashitako hayo matatu ambayo ni Kula njama ya kufanya jinai kesi inayowakabili watuhumuwa wote 30 kosa walilolitenda huko Temeke. 

Kosa la pili ni kufanya mkusanyiko usio halali na kosa la tatu ni kufanya mgomo wa katazo halali la Jeshi la Polisi ambapo kosa la pili na tatu linawakabili mtuhumiwa wa kwanza hadi 28.

Comments

Popular posts from this blog

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO,SAID MECKY SADICKY AFANYA ZIARA KATIKA MAGHALA NA MADUKA YA MARENGA INVESTMENT KUJIONEA HALI YA TATIZO LA SUKARI

CHUO KIKUU CHA MZUMBE WAZINDUA KITUO CHA KUTOA MSAADA WA KISHERIA

MREMA AENDELEA NA MIKUTANO JIMBONI KWAKE VUNJO