WATANZANIA WANG'ARA MBIO ZA NGORONGORO MARATHONI 2015

Waziri mkuu Mstaafu ,Fredrick Sumaye akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wengine mbalimbali wakiwemo waandaji buda mfupi kabla ya kuanza kwa mbio za Km 21 Katika gate la kuingilia hifadhi ya taifa ya Ngorongoro,
Waziri mkuu Msaatfu Fredirick Sumaye akikimbia sambamba na rais wa shirikisho la riadha Tanzania,RT,Athony Mtaka(Kushoto kwake) mkuu wa mkoa wa Arusha ,Daud Ntibenda,pamoja na mkuu wa wilaya ya Karatau Omary Kwaang kuashiria kuanza kwa mbio za Ngorongoro Marathoni.
Maratibu wa Mbio ,Meta Paul akiwa na mmoja wa wasiamamizi ,Leila wakati wakiwaandaa wanariadha kuanza mbio za Km 21 katika lango la kuingilia hifadhi ya taifa ya Ngorongoro.
Mbio zikianza rasmi.
Baaadhi ya washiriki katika mbio hizo ,walikuwemo pia wadhamini kama Maremga Investment,hapa Marenga mwenye truck suit nyeusi akijaribu kukimbiza upepo.
Awawli mbio zikiwa bado ndio zimeanza kundi la wakimbiaji lilionekana wote wanakimbia kwa karibu.
Muda ulivyosonga na hatua ndivyo zilivyo ongezeka.
Hatimaye wakaanza kuachana mmoja baada ya mmoja,
Wengine wakaamua kwenda pamoja ili kupeana moja.
wengine wakafunguka zaidi.
Hatimaye wakapatikana wakimbiaji watatu wakaongoza hadi mwisho wa mbio na hawa ni ,Joseph Theofily(katikati),George Gerald (kulia) na Emanuel Giniki.
Mkimbiaji raia wa Kenya ambaye jina lake halikufahamika mara moja akijaribu kuonesha umahiri wake katika mbio hizo.
Msichana pekee aliyekuwa akiongoza ni Failuna Abdi .
Nyuma ya Failuna alikuwepo Nathalia Elisante.
Mshindi wa kwanza katika Mbio za Ngorongoro Maratahoni 2015 ,Joseph Theofily akimaliza mbio hizo katika uwanja wa Mazingira Bora akitumia muda wa 1:03:09.
Mshindi wa Pili katika mbio hizo ,George Gerald akihitimisha mbio hizo akitumia muda wa 1:03:36
Mshindi wa tatu ,Emanuel Giniki akikalimilisha mbio kwa muda wa 1:03:42.
Giniki akijaribu kupoza koo mara baada ya kumaliza mbio.
Mkimbiaji wa klabu ya riadha ya Holili,Osward Moris akihitimisha mbio.
Mshindi wa kwanza kwa kina dada Failuna Abdi akihitimisha mbio katika nafasi ya kwanza baada ya kutumia muda wa 1 :10:25
Mgeni rasmi katika mbio hizo ,Waziri mkuu Mstaafu ,Fredirck Sumaye akiingia uwanjani huku akihitimisha mbio za km 21 .

Mshindi wa kwanza kwa wanawake,Failuna Abdi akichukuliwa maelezo mara baada ya kumaliza mbio akiwa nafasi ya kwanza.
Mkurugenzi wa Zara Tanzania and Adventures,Zainab Ansel akizungumza na wanahabari katika tamasha hilo.
Meza kuu wakifuatilia mambo mablimbali yanavyoenda uwanjani hapo.
Mkurugenzi wa Zara Tanzania and Adventures,Zainab Ansel akizungumza wakati wa kuhitimisha tamasha la nane la mbio za kimataifa za Ngorongoro Marathoni zilizofanyika Karatu mkoani Arusha.
Baaadhi ya wananchi waliojitokeza katika tamasha hilo.
Rais wa shirikisho la riadha Tanzania (RT) Anthony Mtaka akizungumza katika tamasha hilo.
Waziri mkuu Mstaafu ,Frerick Sumaye akitoa hotuba yake wakati wa tamasha la nane la mbio za kimataifa za Ngorongoro Marathoni zilizofanyika mwishoni mwa wiki Karatu mkoani Arusha.
Mkurugenzi wa Zara Tanzania and  Adventures,Zainab Ansel akitoa zawadi kwa washindi wa mbio za Km 5 upande wa wasichana.
Waziri mkuu mstaafu ,Fredrick Sumaye akizungumza na mshindi wa kwanza mbio za Km 5 kwa upande wa wasichana aliyemaliza mbio bila ya kuwa na kiatu,Sumaye alimpatia zawadi ya fedha kwa ajili ya kununua kiatu.
Umati wa wananchi ukifuatilia matukio mbalimbali katika mbio hizo.
Mkurugenzi wa Zara Tanzania and Adventures ambao ndio waandaaji wakuu wa mbio hizo,Zainab Ansel akikabidhi zawadi kwa mwakilishi wa Bonite Bottlers ambao pia walikuwa wadhamini wa mbio hizo.
Mkurugenzi wa Zara Tanzania and Adventures ambao ndio waandaaji wakuu wa mbio hizo,Zainab Ansel akikabidhi zawadi kwa mwakilishi wa Exim Bank  ambao pia walikuwa wadhamini wa mbio hizo.
Mkurugenzi wa Zara Tanzania and Adventures ambao ndio waandaaji wakuu wa mbio hizo,Zainab Ansel akikabidhi zawadi kwa mwakilishi wa Marenga Investment ambao pia walikuwa wadhamini wa mbio hizo.
Waziri mkuu mstaafu ,Fredrick Sumaye akikabidhi zawadi kwa mkurugenzi wa Zara Tanzania and Adventures kama mwandaji mkuu wa mbio hizo.
Washindi wa mbio hizo kwa upande wa wanawake,
Waziri mkuu mstaafu ,Fredrick Sumaye akimvisha medali mshindi wa kwanza katika mbio hizo,Failuna Abdi.
Waziri mkuu Mstaafu akiwa katika picha ya pamoja na washindi.
Waziri mkuu mstaafu akimvisha medali ,mshindi wa kwanza katika mbio za km 21 kwa upande wa wanaume ,Joseph Theofily,
Waziri mkuu mstaafu akiwa katika picha ya pamoja na washindi kwa upande wa kiume.

Comments

Popular posts from this blog

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO,SAID MECKY SADICKY AFANYA ZIARA KATIKA MAGHALA NA MADUKA YA MARENGA INVESTMENT KUJIONEA HALI YA TATIZO LA SUKARI

CHUO KIKUU CHA MZUMBE WAZINDUA KITUO CHA KUTOA MSAADA WA KISHERIA

MREMA AENDELEA NA MIKUTANO JIMBONI KWAKE VUNJO