Posts

Showing posts from April, 2014

Tizama:KUMBE YANGA WALIANZA MUDA MREFU KUPINGA UBAGUZI WA RANGI

Image
Mshambuliaji wa klabu ya Yanga na timu ya taifa Mrisho Ngasa akila ndizi wakati wa mapumziko katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Panone fc ya mkoani Kilimanjaro.

Tizama:MAJAMBAZI YALIVYO MIMINA RISASI NA KUSABABISHA VIFO VYA ASKARI POLISI WAWILI.

Image
Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP SUZAN KAGANDA akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio la mauaji ya askari Polisi wawili ambao waliuawa wakati wakijitayarisha kukabiliana na Majambazi watatu waliovamia nyumbani kwa mfanyabiashara aliyefahamika kwa jina la IBRAHIMU MOHAMED mkazi wa Ussoke ambapo walipora zaidi ya shilingi milioni moja na laki mbili pamoja na vocha za simu zenye thamani ya shilingi laki moja na ishirini elfu.Kamanda SUZAN alisema majambazi hayo yalikuwa yakitumia bunduki aina ya SMG Baadhi ya askari Polisi wakiutoa mwili wa askari Polisi kwenye Wodi namba moja  aliyeuawa kwa kupigwa risasi na majambazi huko katika Tarafa ya Ussoke wilayani Urambo askari huyo aliyefahamika kwa namba F.5179 PC JUMANNE,walipigwa risasi wakiwa na askari mwenzake ambaye pia alifariki papo hapo namba G.3388 PC SHABAN Mwili wa askari namba F.5179 PC JUMANNE ukipelekwa chumba cha kuhifadhia maiti hospitali ya mkoa wa Tabora Kitete,askari huyo alifariki dunia

Tizama:AJALI YA BASI LA AM ILIYOSABABISHA KIFO CHA MTOTO MKOANI TABORA.

Image
Baadhi ya wananchi katika eneo la Ipuli mkoani Tabora wakishuhudia basi la Am lililopata ajali wakati likiingia mkoani humo likitokea Mwanza. Watoa huduma ya kwanza walifika eneo la tukio ili kuhakikisha wanasaidia majeruhi wa ajali hiyo. Askari Polisi wakisaidiana kubeba mwili wa mtoto aliyegongwa na basi la kampuni ya A.M maeneo ya Ipuli Mnadani ambalo lilikuwa likitokea jijini Mwanza,katika ajali hiyo watu kadhaa wamejeruhiwa. Wananchi wakishuhudia mwili wa mtoto aliyegongwa na basi hilo ambapo walishauri Serikali iliifungie kampuni hiyo ya A.M kuleta mabasi mkoani Tabora ambayo walidai kuwa ni mabovu na yanausalama mdogo kwa wasafiri. Sehemu ya maungio ya Stearing na kiongoza magurudumu ikionekana kama haikuwa salama sana hasa kwa basi kubwa kama hili.

BASI LA AM LAGONGA MWENDESHA BAISKELI ARUSHA.

Image
Mwendesha baiskeli akiwa amelala huku akiwa ameumia vibaya baada ya kugongwa na Basi la AM. Basi la AM linaloanya safari zake katika ya mikoa ya Arusha,Singida na Mwanza limemgonga mwendesha baiskeli ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja. Tukio hilo limetokea asubuhi ya leo katika eneo la Majengo jijini Arusha likihusisha basi hilo lenye namba za usajili T 588 AUT ambapo mwendesha Baiskeri huyo ameumia vibaya.

MAGAZETI YA LEO APRILY 29,2014

Image

MTUHUMIWA MMOJA KESI YA MAUAJI YA BILIONEA WA MADINI AACHIWA HURU.

Image
Na Mwandishi wetu. OFISI ya mkurugenzi wa Mashtaka Nchini imemfutia mashtaka ya mauaji,mmoja  kati ya watuhumiwa nane wa mauaji ya kukusudia dhidi ya mfanyabiashara wa madini ya Tanzanite bilionea , Erasto Msuya (43). Hati ambayo imetumika kumwachia huru Joseph Damas (Chusa) ambaye pia ni mfanyabiashara maarufu wa madini hayo  imetolewa na kusainiwa na mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) Elieza Feleshi na kisha Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuiwasilisha kwa Hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Munga Sabuni . Hati hiyo ambayo hufahamika kama “Nolle Prosecution “ilitolewa mbele ya mahakama hiyo April 16 mwaka huu kwa ajili ya kuingiza rasmi katika kumbukumbu za Mahakama.  “Mheshimiwa hakimu, upelelezi wa kesi hii, umekamilika na ikikupendeza, upande wa mashitaka tunaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kuwasomea washitakiwa maelezo ya mashahidi kabla ya kulipeleka jalada lenye mashitaka haya, Mahakama Kuu kwa ajili ya kuanza kusikilizwa kwa kesi ya mauaji ya kukusudia

RAIS KIKWETE AKABIDHI VITABU 2,181 KWA AJILI YA MAKTABA JESHINI.

Image
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikabidhi vitabu 2069  kwa uongozi  wa Jeshi(JWTZ) kwa matumizi katika maktaba mablimbali za jeshi nchini.Wapili kushoto ni Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange na Watatu kushoto ni Mnadhimu Mkuu Jeshini Luteni Jenerali Samuel Ndomba. -Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na viongozi na makamanda waandamizi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania wakati wa hafla ya kukabidhi vitabu 2069 kwa ajili ya matumizi katika maktaba za jeshi.Vitabu hivyo ni mchango binafsi wa Rais Katika kuboresha mafunzo ya kisasa jeshini(picha na Freddy Maro) Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo katika Ikulu ya Dar es Salaam amekabidhi vitabu 2,181 kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa ajili ya vyuo vya Jeshi ili kuongeza taaluma.   Rais amekabidhi vitabu hivyo kwa Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange na kuahidi kuendelea kutafuta vitabu zaidi kwa ajili ya kuboresha Maktaba ya Jeshi iliyopo katika Chuo Cha Kijeshi kilichopo Monduli, Mkoani Arush