Posts

Showing posts from December, 2014

SAFARI YA MABALOZI KUPANDA MLIMA KILIMANJARO KATIKA SIKU YA KWANZA

Image
Desemba 16 mwaka huu Waziri wa Mambo ya nje ya Nchi ,Mh Benard Membe alikabidhi bendera kwa Balozi Adadi Rajabu kwa niaba ya Mabalozi ,ikiwa ni ishara ya kuanzisha safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro na safari hiyo ilianza kwa muda wa siku sita. Safari ilianza kwa taratibu huku Mabalozi wakitizama mandhari tofauti ya uoto wa asili katika Mlima Kilimanjaro. Safari ya kuelekea Kileleni hivi ndivyo ilivyoendelea kuchukua kasi kwa Mabalozi . Waziri wa mambo ya nje ya nchi ,Mh Benard Membe akioneshwa moja ya kibao kilichokuwa kikielekeza muelekeo wakati wa kupanda Mlima Kilimanjaro. Waziri wa mambo ya nje ya nchi ,Mh Benard Membe akipita katika moja ya daraja kuelekea eneo la Nusu njia. Baada ya kuongoza msafara wa Mabalozi kama ishara ya kuanzisha upandaji wa mlima Kilimanjaro kwa Mabalozi,hatimaye Waziri wa mambo ya nje ya nchi ,Mh Benard Membe alifika eneo la Nusu njia. Waziri wa mambo ya nje ya nchi,Mh Benard Membe akipata chakula na mkuu wa wilaya ya R

VODACOM TANAZANIA YAENDESHA ZOEZI LA KUWAPIMA KIWANGO CHA KILEVI MADEREVA JIJINI ARUSHA.

Image
Askari Polisi wa kikosi cha usalama barabarani ,CPL Miraji Yahaya (kulia) akimpima kiwango cha kilevi,  Manase Temaeli,  dereva wa gari la Machame Safari lenye namba za usajili T 742 BDE ,linalofanya safari zake kati ya miji ya Moshi na Arusha . Askari Polisi wa kikosi cha usalama barabarani ,CPL Miraji Yahaya (kulia) akimpima kiwango cha kilevi , Rumisha  Minja dereva  wa gari la Mtei lenye namba za usajili, T 882 CDU linalofanya safari zake kati ya Arusha na Dar  es Salaam. Askari Polisi wa kikosi cha usalama barabarani ,CPL Miraji Yahaya (kulia)  akipima kiwango cha kilevi kwa  Zakayo Chambo ,dereva wa gari la Kapricon Singida lenye namba  T 134 BSU linnalofanya safari yake kati ya miji ya Singida na Moshi  zoezi lililoratibiwa na kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom zoezi lililoratibiwa na kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom. Asakari wa Kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Arusha wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa kampuni ya Vodacom Tanzania tawi

BENKI YA AZANIA TAWI LA MOSHI LAPITA MITAANI NA KUTOA MKONO WA KRISMASI NA HERI YA MWAKA MPYA KWA WATEJA WAKE

Image
Mkurugenzi wa Idara ya Oparesheni ya Benki ya Azania, Togolani Mramba (wa pili kushoto), akimkabidhi zawadi mmoja wa wateja wakuu wa Benki hiyo mkoani Kilimanjaro, Mfanyabiashara wa Nafaka, Izina Rashid Msangi, ikiwa ni utaratibu wa kawaida wa Benki hiyo kutoa mkono wa shukrani kwa wateja wake na kuwatakia heri katika sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya, wanaoshuhudia ni wafanyakazi wa Benki hiyo, wakiongozwa na Meneja wa Azania Tawi la Moshi, Bi. Hajira Mmambe. Timu ya Wafanyakazi wa Benki ya Azania ikipita mitaani kuwazawadia wateja wao na kuwapa mkono wa Heri ya Krismasi na Mwaka Mpya. Ilikuwa ni msako wa mtaa kwa mtaa, ofisi hadi ofisi, kuhakikisha wateja wote wanapata sababu ya kuendelea kuamini Benki hiyo na kudumisha udugu wa kibiashara. Mkurugenzi wa Oparesheni wa Benki ya Azania makao makuu, Togolani Mramba (wa kwanza kulia) akiwa na timu ya wataalamu kutoka tawi la Moshi, katika ofisi ya Mfanyabiashara wa Mafuta katika Stendi ya Mboya, Manispaa ya Moshi,  Thom