EFTA YACHOCHEA UCHUMI KWA HATI FUNGANI YA BILIONI 50
Mkurugenzi Mtendaji wa Equity For Tanzania Limited- EFTA Bwana Nicomed Bohay akizungumza na wageni waalikwa wakati wa uzindunzi wa Hati Fungani za EFTA tukio lilofanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam katika Hotel ya Kilimanjaro Hyatt Regency. Wageni mbalimbali, wakiwemo wadau wa sekta ya fedha, wawekezaji na wawakilishi wa taasisi za kifedha, wakifuatilia kwa makini tukio la uzinduzi wa EFTA Corporate Bond ya Shilingi bilioni 50, lililofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Uzinduzi huo uliashiria hatua mpya ya kuimarisha upatikanaji wa mtaji wa muda mrefu kwa sekta za uzalishaji nchini. Wajumbe wa jopo la majadiliano wakichangia mada wakati wa uzinduzi wa EFTA Corporate Bond ya Shilingi bilioni 50 jijini Dar es Salaam, wakijadili umuhimu wa mtaji wa muda mrefu katika kuimarisha sekta za uzalishaji na kukuza masoko ya mitaji nchini. Mkurugenzi Mtendaji wa EFTA, Nicomed Bohay, akichangia mjadala wa jopo wakati wa uzinduzi wa Hati Fungani ya Sh bili...