AFYEKA UUME WAKE KUKWEPA USUMBUFU WA WANAWAKE.



Na Mwandishi wetu.


Kijana Ayubu Mnazi Alphonce(24)ambaye amelazwa katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete akipatiwa matibabu baada ya kuamua kujikata uume wake kwa kitu alichodai kuwa ni wembe mpya,sababu za kufanya hivyo Ayubu alieleza kuwa inatokana na usumbufu anaoupata kutoka kwa wanawake ambao amekuwa ana uhusiano nao wa kimapenzi.


MKASA KAMILI:Ayubu ambaye kwasasa amelazwa wadi namba moja katika hospitali hiyo,imeelezwa kuwa baada ya kutokea mfarakano baina yake na mwanamke mmoja ambaye jina halijafahamika aliamua kuingia ndani na kuukata uume wake kwa kutumia wembe mkali na baadae sehemu ya uume huo alikwenda kuutupa kwenye majani na kurudi chumbani kwake.


Taarifa kutoka Jeshi la Polisi zinaeleza kuwa baba  mzazi wa Ayubu baada ya kubaini mtoto wake kuwa amejifungia chumbani kwa muda mrefu akaamua kumgongea mlango na alipopata fursa ya kuingia ndani ndipo akagundua ukweli juu ya jambo hilo na hivyo kumpeleka Ayubu Kituo kikubwa cha Polisi Tabora ambapo jalada la kesi ya kujidhuru lilifunguliwa.


Hata hivyo hali ya Ayubu kwasasa inaendelea vizuri licha ya kuwa amejikata na kubakisha kipande cha sentimeta 5 huku akisubiriwa kufikishwa mahakamani kwa kutenda kosa hilo la kujidhuru mwenyewe pasipo sababu za msingi

Comments

Popular posts from this blog

MGOMO WA WAFANYABIASHARA WATIKISA MKOANI KILIMANJARO.

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO,SAID MECKY SADICKY AFANYA ZIARA KATIKA MAGHALA NA MADUKA YA MARENGA INVESTMENT KUJIONEA HALI YA TATIZO LA SUKARI

MREMA AENDELEA NA MIKUTANO JIMBONI KWAKE VUNJO