Posts

MAALIM SEIF, PROFESA LIPUMBA WAPETA TENA UCHAGUZAI WA CUF, JUMA HAJI DUNI MAKAMU MWENYEKITI

Image
Viongozi wakuu wa CUF wakionyesha mshikamano baada ya kuchaguliwa kukiongoza chama hicho kwa kipindi cha miaka mitano ijayo. Wa pili kulia ni msimamizi wa uchaguzi huo Awadh Ali Said (Picha na Salmin Said, OMKR) Na Hassan Hamad (OMKR)  Mkutano Mkuu wa CUF Taifa umemchagua tena Katibu Mkuu wa Chama hicho kuendelea na wadhifa huo kwa kupata kura 675, sawa na asilimia 99.5 ya kura zilizopigwa.  Mkutano huo pia umemchagua Prof. Ibrahim Lipumba kuwa Mwenyekiti wa CUF Taifa kwa kupata kura 659 sawa na asilimia 95.5 na kumshinda mpinzani wake Chifu Lutalosa Yemba aliyepata kura 30 sawa na asilimia 4 nukta 3.  Aidha mkutano huo umemchagua Mhe. Juma Duni Haji kuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho kwa kupata kura 662 sawa na asilimia 99.25.  Akizungumza baada ya kutangazwa mshindi Katibu Mkuu wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad, amewapongeza wajumbe wa mkutano mkuu kwa kumpa tena ridhaa ya kuongoza chama hicho kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.  ...

Tizama:MWIZI WA PIKIPIKI ALIVYOOKOLEWA NA ASKARI POLISI ,NUSURA WAENDESHA BODABODA WAMTOE ROHO.

Image
Askari polisi wa kituo cha kikuu cha Polisi cha kati akiwa amemshikilia kijana mmoja baada ya kumokoa toka mikononi mwa madereva bodaboda ambao walikwishaanza kujichukulia hatua mkononi kwa kumuadhibu baada ya kutaka kuiba pikipiki. Askari katika ofisi za kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro walilazimika kufunga geti kuzuia kundi kubwa la madereva boda boda na watu wengine wakilazimisha kuingia ili kumfuata mwizi wao wa pikipiki. Madereva hao walionekana kukerekwa na kuzuiwa kumuadhibu kijana huyo na hapa walionekana wakilalamka. Baada ya kuona vijana Mori inapanda geti kabidi lifungwe kabisa. Ikabaki kazi ya kurushiana maneno kati ya wananchi nje ya geti na askari polisi. Maneno yakawa makali zaidi. Jamaa wa nje akatamani kupita katikati ya Nondo hapa. Ni kama jamaa getini alikuwa akimwambia afande wa kike"Umenielewa wewe dada afande"? Geti likafungwa na hakuna mtu aliyepita. Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii kanda ya kaskazini.

MIFUKO YA HIFADHI ZA JAMII YAWAKUMBUKA ASKARI POLISI MOSHI.

Image
Baadhi ya askari polisi wa wilaya ya Moshi wakifuatilia maelezo juu ya mifuko ya hifadhi za jamii. Viongozi wa ngazi ya juu wa jeshi la polisi mkoa wa Kilimanjaro wakifuatilia maelezo juu ya mifuko ya hifadhi ya jamii Baadhi ya asakari polisi wa wilaya ya Moshi wakifuatilia maelezo juu ya mifuko ya hifadhi za jamii. Ofisa mnadhimu namba moja wa jeshi la polisi mkao wa Kilimanjaro SSP Koka Moita akichangia jambo wakati wa semina juu ya mifuko ya hifadhi ya jamii iliyotolewa kwa maofisa wa jeshi hilo wa ngazi mbalimbali. Kamanda wa polisi wa wilaya ya Moshi,OCD Deusdedit Kasindo akizungumza jambo wakati wa semina hiyo. Baadhi ya asakari Polisi wa ngazi na vitengo tofauti walipata nafasi pia ya kuchangia mawazo yao katika semina hiyo. Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii kanda ya kaskazini.

UKWELI KUHUSU UWEPO WA TAARIFA ZA KIFO CHA DK KAWAMBWA HUU HAPA.

TAARIFA TOKA BAGAMOYO Ndg Watanzania, WanaBagamoyo na wapenda maendeleo, kwa niaba ya CCM-Bagamoyo na Ofisi ya Mbunge-Jimbo la Bagamoyo napenda kuleta kwenu Masikitiko yetu kwa niaba ya Chama na Familia ya Mheshimiwa Mbunge Shukuru Jumanne Kawambwa kutokana na Usumbufu ambao umesababishwa na habari zinazoenezwa Mitandaoni kwamba Mheshimiwa Kawambwa amekumbwa na Umauti akiwa njiani anaelekea Mwanza. UKWELI Mheshimiwa Shukuru Jumanne Kawambwa yupo Nchini Canada Akitimiza majukumu yake. Hivyo Watanzania na wana Bagamoyo mnaombwa radhi kwa usumbufu uliotokea na kwamba Mheshimiwa Mbunge yuko na Afya njema na utekelezaji wa Majukumu unaendelea kama kawaida. Ndg.Ridhiwani Kikwete (Mnec) Mbunge - Chalinze

Breaking news:TAARIFA ZISIZO RASMI JUU YA KIFO CHA WAZIRI WA ELIMU DK KAWAMBWA.

Image
 Zipo taarifa zinazoendelea kuzagaa katika mitandao ya simu kadharika kwenye mitandao ya jamii kama Face book na Tweter nk juu ya kifo cha waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi wa Tanzania Dk   Shukuru Kawambwa . Taarifa hizi bado hazijapata chanzo rasmi ingawaje tunaendelea kufanyia kazi ili kujua undani wa swala hili, Jitihada za mwanzo tumejaribu kupiga simu za Mh Kawambwa haziko hewani namba zake zote. Ingawaje zipo taarifa ya kuwa Mh Kawambwa yuko nje ya nchi ,yuko Belgium ,hata hivyo hatutaishia hapo bado ripota etu wako mtaani kufahamu ukweli wa tukio hili endelea kutembelea blogu yako hii ili kujua nini kilichopo juu ya taarifa hii. Taarifa za mwanzo zinadai   alikuwa safarini kuelekea mkoani Mwanza ,taarifa moja wapo inasema amefariki dunia baada ya kupata ajali huku nyingine ikidai amepata mshtuko wa ghafla.Yote kwa yote tutafahaamu hapa hapa.

Tizama:MAHAFALI YA WAHITIMU WA UHIFADHI WA WANYAMAPORI JIJINI MWANZA.

Image
  Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akizindua maabara ya kompyuta katika  chuo cha Taasisi ya Taaluma ya wanyamapori Pasiansi Mwanza wakati wa mahafali ya 49 ya chuo hicho. Kulia ni Balozi wa Marekani Mark Childless. Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu na Balozi wa Marekani Mark Childless wakikagua gwaride la heshima la wahitimu wa chuo hicho.  Wahitimu wa Uhifadhi wa wanyamapori katika chuo Taasisi ya Taaluma ya wanyamapori Psiansi Mwanza wakicheza gwaride juzi, wakati wa  wa mahafali ya 49 ya chuo hicho juzi. Wahitimu wa Uhifadhi wa wanyamapori katika chuo cha Taasisi ya Taaluma ya wanyamapori Psiansi Mwanza wakionyesha ujuzi wa kutumia silaha wakati wa mahafali ya 49 ya chuo hicho juzi. Wahitimu wakionesha utaalamu wa Karate.