Posts

WAFANYAKAZI WA NMB,TAWI LA NELSON MANDELA WATOA MSAADA NA ZAWADI KWA WAGONJWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA KILIMANJARO,MAWENZI.

Image
Kaimu Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Kilimanjaro,Mawenzi Dkt Josephat Boniface akitoa maelzo mafupi kwa wafanyakazi wa Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela waliofika hosptalini hapo kwa ajili ya kutoa zawadi kwa wagonjwa pamoja na msada wa vitendea kazi vya kufanyia usafi kwa hospitali ya Mawenzi. Wafanakazi wa Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela mjini Moshi wakishusha zawadi mbalimbali kwa ajili ya kugawa kwa wagonjwa waliolazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Kilimanjaro,Mawenzi. Meneja wa Benki ya NMB,tawi la Nelson Mandela ,Emanuel Kishosha akimueleza jambo Kaimu Mganga mfawidhi wa hospitai ya Rufaa ya mkoa wa Kilimanjaro,Mawenzi Dkt Josephat Boniface walipofika hospitalini hapo kutoa zawadi kwa wagonjwa waliolazwa. Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro,Mawenzi Dkt Josephat Boniface akieleza changamoto mbalimbali zinazoikabili hospitali hiyo kwa wafanyakazi wa Benki ya NMB tawi la Nelson Mandela walipotembelea wagonj...

RAIS DKT MAGUFULI AMKARIBISHA MFALME MOHAMED VI WA MOROCCO IKULU JIJINI DAR ES SALAAM, MIKATABA 21 YA USHIRIKIANO YASAINIWA

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI wakilakiwa na wafanyakazi pamoja na wageni mbalimbali katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasili.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakipigiwa  ngoma pamoja na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI   mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI   pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa  Ikulu jijini Dar es Salaam kushuhudia uwekaji saini Mikataba ya ushirikiano 21 kati ya nchi hizo mbili.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  na mgeni wake Mtukufu Mfalme wa Morocco Mohamed VI ...