WAFANYAKAZI WA MABENKI MKOANI KILIMANJARO WALIVYOTOANA JASHO KATIKA BONANZA LA BANKERS DAY 2014,

Mashindano ya Mbio yalianza kwa upande wa wafanyakazi wa Benki tofauti tofauti wa Kiume.
Wakimbiaji kwa upande wa kina mama nao walifanya maandalizi na hapa wakiongozwa na Meneja wa Azania Bank ,Hajira Mmambe9mweye kofia nyekundu)
Waratibu wa Bonanza hilo wakijadiliana jambo kabla ya  kufanyika kwa mbio za kina mama.
Mbio za kwa kina mama zikaaanza na kumalizika mshindi wa kwanza na a Mwisho wote wakafahamika.
Wafanyakazi wa Azania Bank wakiwa katika maandalizi ya mchezo wa kusukuma Gogo na hapa wanaongozwa na Meneja wao Hajira Mmambe.
Wafanyakazi wa Uchumi Bank wakiwa katika maandalizi ya mchezo wa kusukuma Gogo .
Benki ya KCB pia walikuwepo kuwakilisha katika mchezo huo.
Kipyenga kikapulizwa shughuli ya kusukuma gogo ikaanza na mshindi akapatikana katika mzunguko wa kwanza Azania Bank wakawa wametakata .
Mzunguko wa Pili wakakutana na wazee wa DTB Bank.
Azania Bank Chali .
Upande wa kufukuza Kuku wazee wa Bacrays Bank nao wakatakata.
Kina mama nao wakamkimbiza Jogoo.
Jogoo akakimbilia chini ya moja ya magarai yaliyokuwepo uwanjani hapo.shughuli ya kumkamata ikaendelea hadi uvunguni mwa gari.
Hatimaye Jogoo akapatikana na mshindi pia akapatikana.
Mwingine yeye aliambulia Manyoya ya mkiani.
Kwenye mbio za Magunia pia wanaume wakaoneshana kazi .
Kina mama nao wakaruka na maguni hadi mshindi akapataikana.
Kazi ilikuwa ni hapa kwenye kuvuta kamba .
Kamba ilikatika zaidi ya mara tatu hali iliyopelekea kushindwa kupatikana kwa mshindi hadi pale walipopunguza idadi ya watu.
Wanaume wakaendelea kuvutana.
Kina mama nao wakavutana .
Kwa upande mpira wa Miguu kikosi cha CRDB Bank kilikuwa imara .
Kikosi kingine kilikuwa ni hiki cha mchanganyiko wa Mabenki wakiwemo wale wa VICOBA.
Mbungi la kufa mtu likapigwa.
Wengine maji mwilini yalikata wakaamua kuongeza.
Hoyaa na mimi niletee moja.
Jamaa akagida migido kadhaa hapa kabla ya  kurudi uwanjani.
Wengine walipatiwa huduma ya kwanza.
Meneja Masoko wa Kampuni ya Megatrade Investment ,Edmund Rutaraka pia alipata nafasi ya kuzungumza neno kama wadhamini wa Bonanza hilo.
Mameneja wa matawi ya Benki zote zilizo shiriki Bonanza hilo wakiwa katika picha ya Pamoja.
Wengine walishindana kucheza dance.
Wengine walishiriki mchezo wa kukaa kwenye kiti.
Zawadi zikatolewa kwa washindi pamoja na vyeti kwa kampuni zilizodhamini Bonanza hilo na benki.

Comments

Popular posts from this blog

MAKATIBU WA CCM VUNJO WASEMA HAWANA UGOMVI NA KATIBU WAO WA WILAYA.

TIB YAKABIDHI MICHORO HALISI YA KITUO CHA MABASI KWA UONGOZI WA MANISPAA YA MOSHI.

BENKI KUU YATOA TAARIFA KUHUSU UPOTOSHAJI JUU YA SARAFU YA SH ,500/