WAFANYAKAZI WA MABENKI MKOANI KILIMANJARO WALIVYOTOANA JASHO KATIKA BONANZA LA BANKERS DAY 2014,
| Mashindano ya Mbio yalianza kwa upande wa wafanyakazi wa Benki tofauti tofauti wa Kiume. |
| Wakimbiaji kwa upande wa kina mama nao walifanya maandalizi na hapa wakiongozwa na Meneja wa Azania Bank ,Hajira Mmambe9mweye kofia nyekundu) |
| Waratibu wa Bonanza hilo wakijadiliana jambo kabla ya kufanyika kwa mbio za kina mama. |
| Mbio za kwa kina mama zikaaanza na kumalizika mshindi wa kwanza na a Mwisho wote wakafahamika. |
| Wafanyakazi wa Azania Bank wakiwa katika maandalizi ya mchezo wa kusukuma Gogo na hapa wanaongozwa na Meneja wao Hajira Mmambe. |
| Wafanyakazi wa Uchumi Bank wakiwa katika maandalizi ya mchezo wa kusukuma Gogo . |
| Benki ya KCB pia walikuwepo kuwakilisha katika mchezo huo. |
| Kipyenga kikapulizwa shughuli ya kusukuma gogo ikaanza na mshindi akapatikana katika mzunguko wa kwanza Azania Bank wakawa wametakata . |
| Mzunguko wa Pili wakakutana na wazee wa DTB Bank. |
| Azania Bank Chali . |
| Upande wa kufukuza Kuku wazee wa Bacrays Bank nao wakatakata. |
| Kina mama nao wakamkimbiza Jogoo. |
| Jogoo akakimbilia chini ya moja ya magarai yaliyokuwepo uwanjani hapo.shughuli ya kumkamata ikaendelea hadi uvunguni mwa gari. |
| Hatimaye Jogoo akapatikana na mshindi pia akapatikana. |
| Mwingine yeye aliambulia Manyoya ya mkiani. |
| Kwenye mbio za Magunia pia wanaume wakaoneshana kazi . |
| Kina mama nao wakaruka na maguni hadi mshindi akapataikana. |
| Kazi ilikuwa ni hapa kwenye kuvuta kamba . |
| Kamba ilikatika zaidi ya mara tatu hali iliyopelekea kushindwa kupatikana kwa mshindi hadi pale walipopunguza idadi ya watu. |
| Wanaume wakaendelea kuvutana. |
| Kina mama nao wakavutana . |
| Kwa upande mpira wa Miguu kikosi cha CRDB Bank kilikuwa imara . |
| Kikosi kingine kilikuwa ni hiki cha mchanganyiko wa Mabenki wakiwemo wale wa VICOBA. |
| Mbungi la kufa mtu likapigwa. |
| Wengine maji mwilini yalikata wakaamua kuongeza. |
| Hoyaa na mimi niletee moja. |
| Jamaa akagida migido kadhaa hapa kabla ya kurudi uwanjani. |
| Wengine walipatiwa huduma ya kwanza. |
| Meneja Masoko wa Kampuni ya Megatrade Investment ,Edmund Rutaraka pia alipata nafasi ya kuzungumza neno kama wadhamini wa Bonanza hilo. |
| Mameneja wa matawi ya Benki zote zilizo shiriki Bonanza hilo wakiwa katika picha ya Pamoja. |
| Wengine walishindana kucheza dance. |
| Wengine walishiriki mchezo wa kukaa kwenye kiti. |
| Zawadi zikatolewa kwa washindi pamoja na vyeti kwa kampuni zilizodhamini Bonanza hilo na benki. |
Comments
Post a Comment