COCA-COLA BONITE YAZIDI KULETA RAHA YA MZUKA WA SOKA NA COKA KANDA YA KASKAZINI

 Washindi wa luninga na pikipiki wakifurahia zawadi zao.
 Washindi wa luninga na pikipiki wakifurahia zawadi zao.
Mmoja wa  washindi wa fedha taslimu akipokea zawadi yake

Wakati mashindano ya kombe la Dunia 2018 yanakaribia, kampuni ya Coca-Cola Bonite Bottlers Limited  ya mjini Moshi inazidi kumwaga zawadi za pikipiki,luninga za kisasa na fedha taslimu  kwa wakazi wa Kanda ya Kaskazini kupitia promosheni ya Mzuka wa Soka na Coka inayoendelea.

Akiongea katika  hafla ya  kukabidhi zawadi kwa washindi  16 wa wiki liyopita, Meneja Mauzo wa Bonite, mkoa wa Arusha Bw. Boniphace Mwasi, alisema zaidi ya wateja 50 wamejishindia zawadi na zawadi bado ziko nyingi. “Bado tunazo zawadi nyingi hivyo natoa wito kwa wakazi wote wa kanda ya kaskazini kuchangamkia kunywa soda za Coca-Cola, ili waweze kujishindia zawadi”.

Wakiongea  muda mfupi baada ya kukabidhiwa zawadi zao washindi waliishukuru kampuni ya Coca-Cola kwa kubuni promosheni zenye mwelekeo wa kuleta furaha kwa jamii hususani kwa kuwakwamua kiuchumi.

Comments

Popular posts from this blog

MGOMO WA WAFANYABIASHARA WATIKISA MKOANI KILIMANJARO.

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO,SAID MECKY SADICKY AFANYA ZIARA KATIKA MAGHALA NA MADUKA YA MARENGA INVESTMENT KUJIONEA HALI YA TATIZO LA SUKARI

MREMA AENDELEA NA MIKUTANO JIMBONI KWAKE VUNJO