Posts

Showing posts from February, 2025

MKURUGENZI MOSHI ATOKWA MACHOZI ,CCM NA CHADEMA WAKIMPA ZAWADI .

Image
Mkurugenzi wa Halmashauriya Manispaa ya Moshi Mwajuma NAsombe akizungumza wakati wa kikao cha mwisho cha Bajeti cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri . Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Zuberi Kidumo akizungumza jambo katika kikao hicho ,kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe . Viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Moshi wakikabidhi keki kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe kama zawadi kutokana na namna alivyosimamia manispaa hiyo pamoja na watendaji wa halmashauri hiyo kufanikisha kupaa kwa mapato ya halmashauri. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe akipokea zawadi ya seti ya vyombo kwa ajili ya chakula kutoka kwa viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Moshi kutokana na namna alivyosimamia manispaa hiyo pamoja na watendaji wa halmashauri hiyo kufanikisha kupaa kwa mapato ya halmashauri. Diwani wa kata ya Kiboriloni Frank Kagoma (Chadema)  akiwaamebeba zawadi ya j...

MAPATO MANISPAA YA MOSHI "YAPAA" KUTOKA BILIONI 6.1 HADI BILIONI 9.9

Image
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Zuberi Kidumo akitangaza ongezeko la mapato ya Halmashauri ya Manispaa ya Moshi . Mkurugenzi wa Hlamshauri ya Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe akizungumza wakati wa baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Moshi . Baadhi ya Wakuu wa Divisheni na watendaji katika ofisi za Halmashauri ya Manipaa ya Moshi wakifuatilia kikao cha Bajeti cha baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo. Baadhi ya Madiwa wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi wakichangia mjdala wa Bajeti ya Halmashauri ya Manispaa ya Moshi wakati wa kikao cha Bajeti .  Na Dixon Hussein - Moshi   Manispaa ya Moshi imepiga hatua kubwa katika ukusanyaji wa mapato ya ndani, ikiongeza mapato kutoka bilioni 6.1 mwaka 2021 hadi bilioni 9.9 mwaka 2025, ongezeko la takribani bilioni 3.7. Mafanikio haya yanatajwa kuwa matokeo ya mikakati madhubuti iliyowekwa ili kuboresha vyanzo vya mapato na kuongeza uwajibikaji katika usimamizi wa rasilimali za umma. Akizungumza katika kikao cha bajeti...