WANAHABARI KILIMANJARO WAPATIWA MAFUNZO YA ONLINE JOURNALISM.

 
Mkufunzi katika mafunzo ya uandishi wa habari wa njia ya mtandao,Bw. Lukelo Mkami akitoa maelezo kwa washiriki wa warsha hiyo inayoendelea katika ukumbi wa KNCU.
 
 
Moshi

 
WAANDISHI wa habari nchini wametakiwa kuhakikisha wanongeza elimu juu ya mabadiliko ya teknolojia ili kuboresha kazi zao za uandishi ziendane na mabadiliko hayo yanayokuwa kila wakati.
 
 

Hayo yameelezwa na mwezeshaji wa mafunzo ya uandishi wa habari kwa njia ya mtandao Bw. Lukelo Mkami yaliyoandaliwa na Muungano wa klabu za waandishi wa habri nchini(UTPC) na kuratibiwa na klabu ya waandishi wa habari mkoani Kilimanjaro(MECKI).

Alisema mabadiliko ya teknolijia yanawalazimisha waandishi wa habari na watanzania kwa ujumla kujifunza kila wakati ili kuendana nayo badala ya kuendelea kutumia mifumo iliyopitwa na wakati.

 
Mwezeshaji huyo alisema mabadiliko yakitumika vyema yanaweza kubadili mifumo ya maisha ya watanzania kutoka kwenye umaskini kwani hutoa elimu, huonyesha fursa za kibiashara na mambo mengine ya maendeleo.

 
“Matumizi ya mitandao kwa baadhi ya watanzania na hata katika nchi zilizoendelea ndio tatizo lakini siyo kwamba kukua kwa teknolijia hakuna shida yoyote matumizi mabaya ndio yanapelekea watu kuona mtandao unashida kubwa”alisema.

 
Aidha Bw. Mkami aliwaasa watanzania kuhakikisha wanasimamia na kudhibiti matumizi ya mtandao kwa watoto wao walio chini ya umri wa miaka 18 badala ya kuingojea serikali kwani hilo ni jukumu la kila mwanajamii ili mtandao utumike katika maendeleo zaidi.

 
“Ni vyema kama familia zikifanya jitihada kwa watoto wao kujua ukuaji wa teknolojia lakini pia matumizi sahihi ya mitandao hiyo ili waweze kukabiliana na mabadiliko hayo na siyo kuwazuia na kungojea matamko ya serikali”alisema

 
Kwa upande wake katibu msaidizi wa MECKI Bw. Dixon Busagaga aliwataka waandishi wa habari nchini kuwa mfano kwa kufanya matumizi sahihi ya mtandao ikiwa ni pamoja kuitumia katika kuboresha kazi zao za kila siku.

 
“Mabadiliko haya ni makubwa kwani kila siku wanasayansi huibua mapya lakini tunapaswa kufuatilia, kujifunza na kujua kwani tunashikilia nafasi kubwa katika jamii ya kuelimisha na zaidi ya hapo”alisema

 
Nao baadhi ya waandishi wa habari walioshiriki katika mafunzo hayo wameiomba UTPC kuona umuhimu wa kuongeza muda wa kozi muhimu kama hizo ili waweze kupata elimu ya kutosha badala ya mfumo unaotumika sasa.
 
Mwisho.
 

Comments

Popular posts from this blog

MGOMO WA WAFANYABIASHARA WATIKISA MKOANI KILIMANJARO.

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO,SAID MECKY SADICKY AFANYA ZIARA KATIKA MAGHALA NA MADUKA YA MARENGA INVESTMENT KUJIONEA HALI YA TATIZO LA SUKARI

MREMA AENDELEA NA MIKUTANO JIMBONI KWAKE VUNJO