MADEREVA WANAOENDESHA VYOMBO VYA MOTO WAKIWA WAMELEWA WAPEWA ONYO


Na Abel Paul wa Jeshi la Polisi

ARUSHA-TANZANIA

Madereva wanaotumia vyombo vya moto wakiwa wamelewa katika Mkoa

wa Arusha wamepewa angalizo endapo watabainika kuendesha magari

hayo wakiwa wamelewa.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa kikosi cha usalama Barabarani Mkoa wa

Arusha mrakibu wa Polisi SP SOLOMON MWANGAMILO wakati

akizumgumza na Madereva wa mabasi mapema leo decemba 30.2022

katika stand kuu ya mabasi yaendayo mikoani na Nchi jirani.

Mwangamilo amesema kuwa dereva atakaye bainika anaviashiria vya

pombe atashugulikiwawa kwa mujibu wa sheria ambapo amewataka

madereva wa magari hayo kutotumia vyombo hivyo wakiwa wameleva.

Ameongeza kuwa kikosi hicho hakimkatazi mtu yeyote kutumia pombe

ambapo amewataka madereva kufuata sheria na taratibu za usalama

barabarani ili kuepuka mkono wa dola.

SP Mwangamilo amesema kuwa dereva atakaye kamatwa kwa makosa

hayo atafungiwa leseni yake na kufikishwa katika vyombo vya sheria kwa

kuhatarisha Maisha ya watu na uharibifu wa miundo mbinu.

Sambamba na hilo amesema kuwa chanzo cha ajali nyingi ni ushabiki wa

mwendo kasi ambapo amewataka madereva hao kuwapuuza

wanaowashawishi kwenda mwendo kasi ili kuepusha ajali za mara kwa

mara.

Kwa upande upande wake Bw. George Emmmanuel ambae ni dereva

amelishukuru Jeshi la Polisi husasani kikosi cha usalama barabarani kwa


kutoa elimu na kuwa kuwakumbusha mambo muhimu ya kuzingatia

Barabarani.


FOOTAGE …………………………………. SP SOLOMON MWANGAMILO

Mkuu wa kikosi cha usalama

Barabarani Mkoa wa Arusha

FOOTAGE …………………………………. BW. GEORGE EMMANUEL

DEREVA

Abel Paul

Afisa Habari wa Jeshi la Paul

0759783894

Comments

Popular posts from this blog

MGOMO WA WAFANYABIASHARA WATIKISA MKOANI KILIMANJARO.

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO,SAID MECKY SADICKY AFANYA ZIARA KATIKA MAGHALA NA MADUKA YA MARENGA INVESTMENT KUJIONEA HALI YA TATIZO LA SUKARI

MREMA AENDELEA NA MIKUTANO JIMBONI KWAKE VUNJO