MFANYABIASHARA MOSHI AGAWA MITAJI YA MIL 10 KWA MARAFIKI ZAKE .

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu akizungumza wakati wa kukabidhi msaada wa bidha mbalimbali kwa kundi la Wafanyabiashara wadogowadogo walioanza Biashara na Mkurugenzi wa Kampuni ya ZAC Enterprisesya mjini Moshi .
Baadhi  ya Wafanyabiashara wadogowadogo katika kundi la Wamachinga 50 walionufaika na msaada kwa ajili ya kukuza mitaji kutoka kampuni ya ZAC Enterprises ya mjini Moshi 
Mkurugenzi wa Kampuni ya ZAC Enterprises Izack Ngowi akioa maelezo kuhusu baadhi ya bidhaa alizokabidhi kama msaada kwa ajili ya kukuza mitaji kwa Wafanyabiashara wadogowadogo maarufu kama Wamachinga alioanza nao biashara.
Baadhi ya Wafanyabiashara wakipokea sehemu ya bidhaa zilizotolewa kwao na Kampuni ya ZAC Enterprises kwa ajili ya kukuza mitaji yao 
Sehemu ya msaada uliotolewa kwa Wafanyabiashara marafiki wa Izack Ngowi ambaye pia ni Mkurugenzi wa kampuni ya ZAC Enterprises kwa ajili ya kukuza mitaji yao.
Baadhi ya wafanyabiashara walionufaika na mtaji kutoka kwa Kampuni ya ZAC Enterprises wakiendelea na biashara baada ya kukuza mitaji yao.
Sehemu ya bidhaa zilizotolewa na Kampuni ya ZAC Enterprises kwa Wafanyabiashara wadogo kwa ajili ya kukuza mitaji yao.

 Na Dixon Hussein- Moshi 

MFANYABIASHARA Izack Ngowi kupitia kampuni yake ya ZAC Enterprises ametoa msaada wa  bidhaa mbalimbali kwa lengo la kuwaongezea mitaji wafanyabiashara wadogo maarufu kama Wamachinga 50 wa mjini Moshi aliokuwa nao wakati wakianza biashara pamoja.

Izack ametoa msaada huo mbele ya Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu ikiwa ni sehemu ya kampuni yake kurejesha sehemu ya faida kwa jamii hususani wafanyabiashara hao ambao wamepatiwa vifaa vya thamani ya sh Mil 10.

“Nimelenga kufanya hivi kwa kuwa mimi hapo kabla pia nilikuwa Mmachinga kama nyie kwa hiyo katika harakati zangu za biashara nikaona ni vyema na mimi niwashike mkono Wamachinga au wafanyabiashara wadogowadogo” alisema Izack.

“Nafanya hivi ili kuongeza mahusianao kati ya brand (Chapa) yetu na wafanyabiashara wadogo wadogo  wamachinga lakini vile vile nimependa kufanya hivi ili kuwaonesha fursa kwamba katika brand (Chapa) yetu ya Zac tuna product ndogo ndogo hizi ni biashara ambazo nyie mnaweza mkafanya ymlango kwa mlango.” Aliongeza Izack.

Alisema lengo jingine la kutoa msaada huo ni kutoa hamasa kwa kundi hilo ili kesho waweze kuwa wafanyabiashara wakubwa ambao wataweza kuwainua vijana wenzao kiuchumi  kwa kuwaajiri na kupunguza kundi la vijana wasio na ajira.

“Nimefanya hivi kutoa hamasa ,leo nyie ni wamachinga lakini kesho mnaweza mkawa  wafanyabiashara wakubwa ,wafanyabiashara wote wakubwa kunasehemu walitoka ,walianzia  wakafanya kazi kwa bidi wakatengeneza mahusisno mazuri na watu wakapata mitaji wakawa wakubwa” alisema Izack.

Akiizungumza baada ya kukabidhi msaada huo ,Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu aliyekuwa mgeni rasmi amepongeza hatua ya mfanybiashara Izack kukumbuka uhitaji wa vijana wenzake katika kujikwamua kiuchumi

“Kutoa ni moyo na wala sio utajiri ameeleza hapa kwa kifupi kwamba yeye alikuwa miongoni mwa wamachinga ambao na yeye anatembeza vitu barabarani kwa hiyo ametembeza kwa malengo akawekeza kidogo kidogo hatimaye leo amekuwa mfanyabiashara wa kati “alisema Babu .

“Izack ameamua kumuunga mkono Mh Rais kwa vitendo na ndugu zangu kutoa mtaji wa milioni kumi kwa ajili ya kuwakabidhi nyinyi ndugu zake ambao mmeanza naye kazi ,yeye  Mungu akamjalia akafika hatua aliyofika sio jambo rahisi  inataka moyo sana.” Aliongeza Babu.

Alisema mfanyabiashara Izack kaamua kutoa vifaa vya milioni 10 kwa ajili ya kuwapa ndugu zake ambao walihangaika pamoja ni jambo la nadra sana kuona watu waliofanikiwa ama wafanyabiashara wanawakumbuka watu walioanza nao.

“Kwa hivyo nataka muige sasa yeye anatoa vifaa vya milioni kumi na nyie ambao mnafanya biashara pamoja na ile mitaji yenu hakikisheni sasa mnaweka mitaji yenu vizuri ili nanyie mmfikie kama alivyofika yeye.” Alisema Babu.

 

Aidha Babu alipongeza hatua ya wafanyabiashara wa mkoa wa Kilimanjaro kuendelea na biashara zao bila ya kufunga maduka na kwamba hata kama zipo changamoto zinazowakabili serikali itaendelea kuzitatua kwa wakati.

“Ndugu zangu nyie mnajitafutia riziki kwenye maeneo mbali mbali na hatutaki serikali kuwabugudhi lakini na nyie lazima mtii sheria bila shuruti yani mkiambiwa hapa ndio maeno ya wafanyabiashara ndogondogo wamachinga basi mjue ndio hapo hasa mkiondoka mkienda kwenye maeneo mengine ndo ugomvi” alisema Babu .

“Juzi miliona watu wa Musoma mliona sasa hayo siyataki kwneye mkoa wangu wa Kilimanjaro nataka mkiambiwa mfanyebiashara hapa basi mtiii lakini changamoto zenu DC amezisema naye ndio mkuu wenu wa wilaya atazishuhghulikia kama kuna jambo amablo nyie mnaona je serikali imewapa eneo ambalo halifikiki na wananchi hawafiki hamfanyi biashara DC atatafuta utaratibu mwingine “ ALIONGEZA babu.

Naye mkuu wa wilaya ya Moshi Zephania Sumari amesema tayari wamepanga kukutana na kundi la wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama Wamachinga ili kuangalia namna gani wanaweza kutatua changamoto zilizopo na kuzipatia ufumbuzi.

“Nimeweza kukutana na ninyi wafanayabiashara wadogo wadogo maarufu kama Wamachinga ,Mh Mkuu wa mkoa hawa sio wageni kwangu nimeshakutana na viongozi wao wa mkoa nimekutana na viongozi wao wa wilaya na waliongea baadhi ya changamoto nina furaha kukujulisha kwamba hawana changamoto nyingi “alisema Babu.

Kampuni ya ZAC Enterprises inayosambaza vifaa mbalimbali vya umeme pamoja na simu za mkononi tayari imekabidhi vifaa hivyo kwa walengwa ikiwa ni awamu ya kwanza na kwamba itaendelea na utaratibu huo mara kwa mara .

Mwisho .

 

 

Comments

Popular posts from this blog

MAKATIBU WA CCM VUNJO WASEMA HAWANA UGOMVI NA KATIBU WAO WA WILAYA.

TIB YAKABIDHI MICHORO HALISI YA KITUO CHA MABASI KWA UONGOZI WA MANISPAA YA MOSHI.

BENKI KUU YATOA TAARIFA KUHUSU UPOTOSHAJI JUU YA SARAFU YA SH ,500/