WANAFUNZI TPC WADANDIA “KIBERENGE “CHA MIWA KURUDI MAKWAO ,ABC IMPACT WATOA BAISKELI .

 

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya TPC wakionesha furaha yao wakati wakiendesha baiskeli zilizotolewana taasisi ya ABC Impact kama sehemu ya msaada ukilenga kuondoa changamoto ya usafiri kwa wanafunzi wanaoishimaeneo ya mbali na shule .
Wanafunzi wa kike ndio wamekuwa walengwa wakubwa wa msaada wa Baiskeli uliotolewa na taasisi ya ABC katika kuwapunguzia changamoto yakutembea umbali mrefu pamoja na vishawishi ambavyo vingeweza kuchocheakushindwa kuendelea na masomo .
Mgeni rasmi katika hafla ya kukabidhi Baiskeli kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondariya TPC ,Diwani wa kata ya Arusha chini Lenard Waziri (Mwenye suti nyeusi) akikata utepe ikiwa ni ishara ya kupokea msaada wa Baiskeli uliotolewa na taasisi ya ABC Impact.kulia kwake ni Ayanna Kimaro mkurugenzi wa taasisi ya ABC Impact 
Mgeni rasmi katika hafla ya kukabidhi Baiskeli kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondariya TPC ,Diwani wa kata ya Arusha chini Lenard Waziri (katikati) akiendesha Baiskeli kama ishara ya kupokea msaada huo kutoka kampuni ya ABC Impact.
Mgeni rasmi katika hafla ya kukabidhi Baiskeli kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondariya TPC ,Diwani wa kata ya Arusha chini Lenard Waziri akizungumza wakati wa hafla fupi ya kupokea msaada wa Baiskeli kutoka kampuni ya ABC Impact.
Mkurugenzi wa Kampuni ya ABC Impact Ayanna Kimaro akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi msaada wa Baiskeli kwa wananfunzi ikiwa ni sehemu ya programu ya kupunguza changamoto kwa wafunzi wanaosoma shule zilizo mbali na makazi yao.
Baadhi ya Wanafunzi wakifuatilia kwa karibu tukio hilo .
Sehemuya Msaada wa Baiskeli zilizotolewana Taasisi ya ABC Impact kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari ya TPC .
Mwanafunzi Paschal Paul akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wenzake mara baada ya kukabidhiwa msaada wa Baiskeli kutoka Taasisi ya Impact .
Baadhi ya Wazazi waliofika shuleni hapo kushuhudia makabidhiano ya msaada wa Baiskeli kwa wanafunzi wa shule ya sekondari ya TPC ambao ni watoto wao.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya TPC Salehe Shekibwai akitoa neno la shukurani kwa msaada wa Baiskeli uliotolewa kwa wanafunzi wa shule hiyo na taasisi ya ABC Impact .
Sehemu ya msaada wa Baiskeli ulitolewa na Taasisi ya ABC Impact kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari ya TPC .
Sehemu ya msaada wa Baiskeli ulitolewa na Taasisi ya ABC Impact kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari ya TPC .

Na Dixon Hussein - Kilimanjaro

Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari TPC iliyopo wilaya ya Moshi mkoa wa Kilimanjaro wanatajwa kuwa katika hali ya kuhatarisha maisha kutokana na tabia ya kudandia Garimoshi (Treni), maarufu kama Loko wakati wa kwenda na kurudi shuleni.

Hayo yamebainishwa na baadhi ya wanafunzi pamoja na walimu wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa  mpango wa kusaidia wanafunzi wa kike wanaosoma shule ambazo ziko mbali na mahala wanapoishi,mpango unaratibiwa na taasisi ya ABC Impact .

Wanafunzi hao wanadaiwa kutumia treni ambazo zimekua zikitumika kubeba miwa kutoka mashambani kupeleka kiwandani hatuainayotajwa kuwa ni hatarishi kwa maisha yao hasa kwa wanafunzi wakike .

Katika jitihada za kuboresha usafiri wa wanafunzi wa kike na kupunguza changamoto wanazokumbana nazo wakati wa kwenda shule, taasisi ya ABC Impact imetoa msaada wa baiskeli kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari TPC.

Hii ni sehemu ya mpango wao wa kusaidia wanafunzi wanaotembea umbali mrefu kufika shuleni kwa wakati na kuongeza ufanisi wao katika masomo.

Akizungumza wakati wa hafla ya ugawaji wa baiskeli hizo, Mkuu wa Shule ya Sekondari TPC Salehe Shekibwai amesisitiza kuwa msaada huu ni fursa muhimu kwa wazazi kushiriki katika kuwawezesha watoto wao kupata usafiri salama.

“ABC Impact wameonyesha moyo wa upendo kwa kugawa baiskeli hizi, lakini wazazi pia wanapaswa kushiriki kwa kuchangia sehemu ya gharama. Hili litawafanya wanafunzi kuthamini baiskeli wanazopata,” alisema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Taasisi ya ABC Impact Ayanna Kimaro alieleza kuwa lengo lao ni kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapata usafiri wa uhakika ili kuepuka changamoto zinazoweza kuathiri elimu yao, ikiwa ni pamoja na kuchelewa kufika shuleni na hatari za barabarani kama kuomba lifti kwa magari yasiyo salama.

 “Tunataka kuona kila mwanafunzi anapata fursa ya kusoma bila kikwazo cha usafiri. Tunaamini kuwa kila baiskeli tunayotoa ni mbegu ya mafanikio kwa mtoto wa Kitanzania,” aliongeza mkurugenzi Ayyana.

Mmoja wa wanafunzi walionufaika na msaada huo Paschal Paul alieleza furaha yake kwa kupokea baiskeli, akisema itamsaidia kufika shuleni kwa wakati na kuwa na muda wa kutosha kwa masomo na shughuli nyingine za kielimu.

“Zamani nilikuwa nikichelewa kufika shuleni kutokana na umbali mrefu, lakini sasa nitakuwa nakuja kwa wakati,” alisema mwanafunzi huyo.

Diwani wa kataya Arusha Chini Leonard Waziri  alitoa pongezi kwa Taasisi ya ABC Impact kwa hatua yao ya kusaidia sekta ya elimu kupitia usafiri.

Alibainisha kuwa wazazi wanapaswa kuunga mkono juhudi hizo kwa kuhakikisha kuwa wanafunzi wanazitunza baiskeli hizo na kuzitumia kwa malengo yaliyokusudiwa.

Pia Waziri alisisitiza umuhimu wa usalama wa barabarani kwa wanafunzi, akiwataka kutumia baiskeli zao kwa tahadhari kubwa ili kuepuka ajali.

Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na walimu, wazazi na viongozi wa jamii, ambao kwa pamoja walikubaliana kuwa msaada huu utakuwa na manufaa makubwa kwa elimu ya watoto wa kike na kuwapunguzia mzigo wa kutembea umbali mrefu kila siku kwenda shuleni.

Mwisho 



Comments

Popular posts from this blog

TIB YAKABIDHI MICHORO HALISI YA KITUO CHA MABASI KWA UONGOZI WA MANISPAA YA MOSHI.

CHUO KIKUU CHA MZUMBE WAZINDUA KITUO CHA KUTOA MSAADA WA KISHERIA

MAKATIBU WA CCM VUNJO WASEMA HAWANA UGOMVI NA KATIBU WAO WA WILAYA.