WANAWAKE WA TAASISI YA UTAFITI WA MBOGA DUNIANI WAPELEKA TABASAMU MOTONYOK ARUSHA .

Wanawake katika katika Taasisi ya Utafiti wa Mboga Duniani “World Vegetable Center” iliyopo Tengeru jijini Arusha wakionesha furaha yao muda mfupi kabla ya kuanza safari ya kwenda kituo cha kulea watoto wanaoishi katika mazingira cha Motonyok kupeleka msaada wa elimu wa namna ya kuotesha mboga .
Baadhi ya Wanawake katika taasisi ya Utafiti wa Mboga Duniani “World Vegetable Center” iliyopo Tengeru jijini Arusha wakiwa wamebeba miche ya miti ambayo kwa ajili ya kuoteshwa katika kituo cha kulea watoto wanaotoka katika mazingira hatarishi cha Motonyok kilichopo Olasiti jijini Arusha.
Mkurugenzi wa taasisi ya Utafiti wa Mboga Duniani “World Vegetable Center” iliyopo Tengeru jijini Arusha Bi Colleta Ndungulu (katikati) akiwa na Mkurugenzi wa kituo cha kulea watoto wanaotoka katika mazingira hatarishi cha Motonyok Bi. Emmy Nicholaus Sitayo ,wakati wanawake wa taasisi hiyo walipotembelea kituo hicho kutoa mafunzo .
Baadhi ya Wafanyakazi katika taasisi ya utafiti wa Mboga Duniani (World Vegetable Center) wakifuatilia matukio yaliyokua yakiendelea katika kituo hicho ,walipoenda kuwatembelea watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi .
Mkurugenzi wa taasisi ya Utafiti wa Mboga Duniani “World Vegetable Center” iliyopo Tengeru jijini Arusha Bi Colleta Ndungulu akizungumza wakati wanawake katika taasisi yake walifika kituo cha kulea watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi walipofika kituoni hapo kutoa elimu juu ya kilimo cha mboga .
Mkurugenzi wa kituo cha kulea watoto wanaotoka katika mazingira hatarishi cha Motonyok Bi. Emmy Nicholaus Sitayo akizungumza wakati wanawake katika taasisi ya Utafiti wa Mbiga Duniani walipofika katika kituo cha kulea watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi walipofika kituoni hapo kutoa elimu juu ya kilimo cha mboga .

Baadhi ya Wafanyakazi katika taasisi ya utafiti wa Mboga Duniani (World Vegetable Center) wakifuatilia matukio yaliyokua yakiendelea katika kituo hicho ,walipoenda kuwatembelea watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi .
Sehemu ya msaada wa Chakula ,Sukari Sabuni ,Unga ,Dawa ya meno pamoja na nguo zilizotolewa na Wanawake katika taasisi ya utafiti wa Mboga Duniani (World Vegetable Center) kwa ajili ya watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi wa kituo cha Motonyok kilichopo Olasiti jijini Arusha .

WANAWAKE WA TAASISI YA UTAFITI WA MBOGA DUNIANI WAPELEKA TABASAMU MOTONYOK ARUSHA .

Na Dixon Hussein – Arusha

WANAWAKE katika Taasisi ya Utafiti wa Mboga Duniani “World Vegetable Center” iliyopo Tengeru jijini Arusha wame wameacha tabasamu kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi wa kituo cha Motonyok baada ya kukabidhi zawadi ya vitu mbalimbali ikiwemo Mchele ,Sukari,Sabuni pamoja na nguo kama sehemu ya msaada kwa watoto hao

Huu ni utaratibu wa kawaida kwa taasisi hii iliyojipambanua katika tafiti za mboga kutumia watafiti wake kama sehemu ya maadhimisho mwezi wa kumbukumbu ya siku wanawake Duniani,maadhimisho ambayo hufanyika kila mwaka kote duniani.

Akizungumza baada ya kukabidhi msaada huo Mkurugenzi wa taasisi ya World Vegetable Center Colleta Ndunguklu amewapongeza waanzilishi na walimu wa kituo hicho kwa kutoa huduma ya malezi na elimu kwa Watoto waishio katika mazingira magumu na wenye ulemavu.

Amesema kuwa Wanawake wa Taasisi ya World Vegetable Center wameguswa na kuamua kutoa msaada huo kwa kuwa wanatambua mchango unaofanywa na Familia hiyo.

“Taasisi yetu inakupongeza Sana wewe na Familia yako kwa kuliona hili la kuhudumia Watoto wenye uhitaji, Wanawake wengi wanatelekeza Watoto kwa sababu ya kukosa uvumilivu wa kuhudumia Watoto wenye mahitaji maalumu” amesema Colleta.

“ Sisi tunatoka kwenye taasisi ya mbogamboga ,tunafanya utafiti kwenye mboga ili kupata mbegu bora  ,tunamshukuru kwa kutukaribisha hapa, tumesikia mengi kutoka kwenu  pia wewe ni mama bora  una mikoba mingi sana, mkoba wa kuwa mama, mkoba wakuwa mlezi , mkoba wa kuwa mwalimu” alisema Colleta

Mkurugenzi wa kituo cha kulelea Watoto waishio katika mazingira magumu cha Matonyo Bi. Emmy Nicholaus Sitayo amesema kituo hicho kilianzishwa kwa lengo la kupunguza vitendo vya ukatili vinavyofanyiwa baadhi ya Watoto yatima na waishio mitaani ikiwemo ubakaji, kupigwa na kunyimwa haki za msingi za binadamu.

Amesema kituo hicho kilianzishwa mwaka 2006 kikiwa na watoto tis ana sasa kinahudumia watoto waliopo shuleni Hamsini na nane ,wasichana wakiwa ni thelathini na wavulana ishirini na nane.

“Watoto waliopo kituoni ni 58 kati ya hao  10 tayari wameshavuka wapo elimu ya Sekondari na wengine ndo hawa tuliona nao hapa  na shule yetu ilitakiwa iwe na watoto 400 na mpaka leo tuna watoto 125”alisema Sitayo  .

“Tunaamini tutafika hatuombi tupate yatima au watoto wenye mazingira magumu tunatamani wapungue ili wawe na walezi na hapa tuna kitengo pia cha kulea watoto wenye changamoto ya ulemavu tunawasaidia na tukisikia mahall  wanatoa elimu tunawapeleka” aliongeza Sitayo . 

Sitayo ameshukuru ujio wa taasisi hiyo katika kituo hicho na msaada uliotolewa kwa watoto hao pamoja na elimu ya uandaaji wa shamba na uoteshaji wa mboga jambo ambalo amelitaja kuwa ni kubwa kuwafanya watoto wajisikie kuwa ni kundi linalo thaminika katika jamii.

“Tunaomba Muendeleze Moyo huo wa Upendo kwa Watoto wenye uhitaji” amesema Bi Sitiya

Mwisho 


Comments

Popular posts from this blog

TIB YAKABIDHI MICHORO HALISI YA KITUO CHA MABASI KWA UONGOZI WA MANISPAA YA MOSHI.

CHUO KIKUU CHA MZUMBE WAZINDUA KITUO CHA KUTOA MSAADA WA KISHERIA

MAKATIBU WA CCM VUNJO WASEMA HAWANA UGOMVI NA KATIBU WAO WA WILAYA.